Wateja wengi huuliza maswali yanayofanana kuhusu routers na huduma za intaneti tunazotoa. Hapa tumekusanya baadhi ya maswali maarufu pamoja na majibu yake:
❓ 1. Router ni nini?
📡 Ni kifaa kinachoruhusu vifaa kama simu, laptop, au Smart TV kuunganishwa na intaneti bila waya (Wi-Fi).
❓ 2. Ni vifaa vingapi vinaweza kuunganishwa na router moja?
✅ Kulingana na aina ya router, unaweza kuunganisha kuanzia vifaa 5 hadi 30 bila kupungua kwa kasi.
❓ 3. Router inafanya kazi muda gani?
🕒 Router inafanya kazi 24/7 muda wote ilimradi kuna umeme au power bank kwa walioko maeneo ya umeme wa uhakika mdogo.
❓ 4. Je, router inahitaji laini ya simu?
📲 Ndio, nyingi hutumia line ya mtandao kama Vodacom ili kupata intaneti. FreshTech tunakusaidia kuseti kila kitu.
❓ 5. Nifanyeje nikihitaji router au msaada wa kuunganisha?
📞 Piga 076 6079 000. Tutakushauri, kukuletea, na kukufungia router bila usumbufu.
🛠️ FreshTech – Huduma Kamili za Intaneti
Tunakuunganisha kwa urahisi, haraka, na kwa bei nafuu.

0 Comments